Kwanini Afrika inamlilia Fidel Castro
Mwalimu Nyerere akiwa na Fedel Castro wakati wa uhai wao. Na LEAH H. MWAINYEKULE, DESEMBA 10, 2013 wakati dunia nzima ikiwa inafuatilia matangazo ya moja kwa moja ya kumbukumbu ya kifo cha Rais Nelson Mandela, jambo la kihistoria lilifanyika: Rais Barack Obama wa Marekani alishikana mkono na Rais Raul Castro wa Cuba. Wakati huo huo, Seneta Ted Cruz wa Marekani, alitoka nje wakati Raul Castro aliposimama kutoa hotuba kwenye tukio hilo. Rais Obama alikuwa Rais wa pili wa Marekani kuushika mkono wa kiongozi wa Cuba, katika kipindi cha miaka 60. Mwaka 2000, Rais Bill Clinton alishikana mikono na kaka wa Raul ambaye alikuwa kiongozi wa Cuba wakati huo, Rais Fidel Castro. Hilo lilitokea wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa huko New York na Wamarekani wengi walitoa shutuma kutokana na mkono huo. Tukio la Rais Obama kusalimiana kwa mkono na Raul Castro, liliripotiwa kwa kiasi kikubwa na vyombo vya habari vya nchi za Magharibi....